
“Peter, Je, Unasikia Muziki?”
Rais aonekana kwenye filamu ya kurekodiwa ya "Royal Tour"
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan alionyesha ujasiri, ushujaa na kipaji cha kuigiza kama mwongoza watalii kwa nchi yake.
Ikulu ya White House mjini Washington, Jumba la Sanaa la Guggenheim mjini New York na Youtube zilitandaza zulia jekundu kwa ajili ya “Mama Samia'' akicheza nafasi kuu katika filamu ya utalii ya saa moja kuhusu Tanzania na Zanzibar. Filamu hiyo iitwayo “The Royal Tour'' inamfuata Hassan na mtayarishaji maarufu wa Marekani Peter Greenberg wakisafiri nchini nzima kutoka tamasha la Taarab katika Ng.
“Napenda kuwatazama wapenzi wakitembea wakiushikana mikono kando ya ufuo,” asema rais akiwa Forodhani. Kuhusu nafasi yake mpya anasema: “Sikuwahi kutarajia kuwa rais”, kuhusu nchi yake: ”Wengine hawaamini kuwa mwanamke anaweza kuchukua nafasi ya juu namna hii.” Akitembelea msikiti wa nyumbani kwao Kizimkazi, alipokulia miongoni mwa ndugu 14, anasema “dini ilinifundisha kuhusu haki za wasichana.’
Kwa sauti yake laini na nzito, kiongozi wa taifa la Kiislamu, ambaye hubadilisha mavazi kila tukio lakini haonekani kamwe bila skafu ya kichwa au rangi ya midomo, ni msimulizi wa ajabu. Katika tukio moja anamwendesha Greenberg kuzunguka Serengeti akimkumbusha taswira ya Malkia Elizabeth wakati wa matembezi yake kwa Land Rover nchini Uskoti: "Ilikuwa mara yangu ya kwanza kuendesha gari kwa miaka 15," alisema Hassan huko Washington. Greenberg amefanya vipindi maalum vitano vya televisheni vya Ziara ya Kifalme, na kimoja tu kilichobaki katika Africa, nchini Rwanda.
Uchez"
Makala Zinazohusiana

Iftar ya Jamii katika Fumba Town

Taarifa ya umma kutoka CPS Africa

Nyumba Nzuri Ya Vyumba Viwili

Nyumba ya kifahari ya vyumba 3 ya kipekee yenye bwawa

Ghorofa maridadi ya vyumba vitatu vya kulala



