
Okoa bahari, vaa wavu
Likizo ya Zanzibar yazua biashara kubwa ya kijani kibichi Ulaya
Wakati wa ziara ya wiki tatu visiwani Zanzibar, wanandoa wa Ujerumani waligundua dhamira yao na kuanza kugeuza nyavu za zamani za samaki kuwa „vikuku vya kufunga“.
Hivi sasa Madeleine von Hohenthal na Benjamin Wenke wameuza zaidi ya vifaa 100,000 vya kijani mtandaoni. Pamoja na mashirika washirika wa kimataifa wameokoa tani zaidi ya 700 za nyavu zilizotupwa katika bahari duniani kote.
“Yote ilianza kwa kupiga mbizi kando ya pwani nzuri ya Zanzibar mwaka 2015,” anakumbuka Benjamin Wenke, nilipomkuta mjini Hamburg, Ujerumani ambapo biashara hiyo ina makao yake. “Tuligundua vipande vya nyavu za zamani za uvuvi, zikielea majini, zikileta hatari kubwa kwa mazingira.”
Hata hivyo, wavuvi wa Zanzibari walikuwa wepesi kusema, kwamba nyavu nyingi hazikutupwa huko nyumbani bali zilitoka kwa meli kubwa za uvuvi – “tatizo kubwa duniani” kama walivyogundua wenzi hao waliotembelea. “Tulirudi Ujerumani tukiwa na kipande cha wavu kilichofungwa mikononi mwetu,” mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 37 anasimulia na “kuendelea kuota ndoto kuhusu nini cha kufanya nacho.”.
“Si mengi yaliyojulikana kuhusu suala hilo mwaka 2015,” anasema - na akaanza kutafiti. Matokeo yake: Kila mwaka, tani milioni moja za nyavu za uvuvi hupotea au kutupwa baharini. Zinapoteza madhumuni yake, lakini si uwezo wake wa kazi - na huendelea kuvua zikiwa zinazama baharini. Mamia ya maelfu ya wanyama wa baharini hunaswa katika kinachojulikana kama “ghost nets” na hupata kifo cha kikatili. Nyavu hizo pia huunda asilimia 40 ya eneo maarufu la "Great Pacific garbage patch," mojawapo ya maeneo makuu matano ya takataka za plastiki katika bahari zetu.
„"Ni wakati wa kumaliza hili," Benjamin na Madeleine walifikiri, na – wakiwa na uzoefu wa kitaalamu katika masoko na ubunifu – walianza kujaribu kutumia upya taka za baharini kuwa bidhaa mpya kama kamba za mbwa, vifungo vya funguo, pete na mifuko. Kila kitu kinatengenezwa kwa mikono katika warsha huko Hamburg. Bidhaa yao inayouzwa zaidi ilikuwa kile wanachokiita braseneti (kutoka mkanda wa mkono na wavu), ambayo sasa wanauza matoleo kadhaa mtandaoni pamoja na cheti cha asili – kwa kila kipande kwa 25$.
Je, wapenzi hao, ambao kwa sasa wamefunga ndoa na wenye kiburi cha kumzaa mwana wao Eden mwenye umri wa miaka miwili, wamerejea katika chanzo cha wazo la biashara yao, Zanzibar? “Bado hatujarejea,” wanasema, “lakini tunapanga.”
Habari na maagizo: bracenet.net
Makala Zinazohusiana

Iftar ya Jamii katika Fumba Town

Taarifa ya umma kutoka CPS Africa

Nyumba Nzuri Ya Vyumba Viwili

Nyumba ya kifahari ya vyumba 3 ya kipekee yenye bwawa

Ghorofa maridadi ya vyumba vitatu vya kulala



